Wanafunzi 7 wafariki dunia katika mkasa wa moto Shule ya Sekondari, Nairobi

Image result for picha za ajali ya moto

Takribani wanafunzi 7 wamefariki dunia huku wengine 10 wakijeruhiwa kufuatia moto uliozuka saa nane za usiku katika bweni la shule ya wasichana ya Moi mjini Nairobi,nchini Kenya 

Akizungumza na vyombo vya habari nchini Kenya waziri wa Elimu Dr,Fred Matiang'i amethibitisha kuzuka kwa moto huo na kudai kuwa chanzo cha moto huo bado hakijajulikana lakini tayari idara zote muhimu za uchunguzi zimewasili shuleni hapo kubaini chanzo cha moto huo.
Majeruhi kumi wakiwemo wawili mahututi wamekimbizwa katika hospitali ya Kenyatta mjini humo.
Aidha serikali imetoa salamu za pole na rambirambi kwa wazazi waliopoteza watoto wao katika mkasa huo ulioikumba shule hiyo na kuahidi kushirikiana nao katika kipindi hiki kigumu.
Shule hiyo imefungwa kwa majuma mawili kufuatia mkasa huo.


Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.