WAAMKA USIKU WA MANANE KUSAKA HUDUMA YA MAJI.
Related image
hivi ndivyo lilivyokubwa tatizo la uhaba wa maji
Wananchi wa kijiji cha Kasera kata ya Nyakaliro halmashauri ya Buchosa wamelazimika kuamka usiku wa manane kusaka huduma maji  baada ya vyanzo vya maji  walivyokuwa wakitumia  kukauka.
Wakizungumza na Radio sengerema baadhi ya wanawake wa kijiji hicho wamesema wanapata shida kupata maji na inawalazimu kuamka usiku wa manane kutafuta maji jambo linalopelekea upotevu wa vyombo pamoja na vitisho mbalimbali.
Naye   diwani wa kata hiyo Mh, Kalunga Ibrahim amekiri kuwepo kwa changamoto hiyo katika vijiji mbalimbali vilivyopo   katika kata yake  licha ya kuwepo chanzo cha maji   kinachosambaza maji kwenda  kata ya  Nyehunge.   
Kwa upande  wake    mbunge wa Jimbo la Buchosa Dkt, Charles Tizeba kupitia mkutano wake wa hadhara na wananchi wa kijiji hicho amesema haitafika    mwaka 2020 kijiji hicho kitakuwa na umeme.
Na Elisha Magege.



Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.