Uhuru Kenyatta apinga uamuzi wa mahakama

Image result for picha ya uhuru kenyatta
Aliyekuwa Rais mteule wa Kenya Uhuru Kenyatta ,ametoa msimamo wake juu ya uamuzi wa mahakama uliotolewa leo wa kurudiwa kwa uchaguzi wa urais, na kusema kuwa hakubaliani nao ingawa anaheshimu uamuzi huo.

Akizungumza katika Ikulu ya Kenya muda mfupi baada ya uamuzi wa mahakama kutolewa, Uhuru Kenyatta amesema anaheshimu uamuzi uliotolewa na mahakama wa kufuta matokeo ya uchaguzi yaliyompa ushindi, lakini hakubaliani na uamuzi huo.
Pamoja na hayo Uhuru Kenyatta amesema kwa kuwa wanaheshimu uamuzi wa mahakama, wako tayari kurudi kwenye kampeni na kupiga kura tena kama ambavyo mahakama imetaka.

Leo asubuhi Makama ya juu zaidi ilitoa uamuzi wa kesi ya uchaguzi iliyofunguliwa na muunganiko wa vyama vya upinzani nchini Kenya (NASA) dhidi ya Tume ya Uchaguzi iliyosimamia uchaguzi huo ambao Uhuru Kenyatta aliibuka mshindi, na kuamua kufuta matokeo hayo huku ikitaka urudiwe baada ya siku 60.


Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.