UGONJWA WASHAMBULIA ZAO LA MUHOGO
Image result for picha ugonjwa wa zao la muhogo
picha ya zao la muhogo
                              
Wakulima wa zao la muhogo wametakiwa kulima kwa kufuata ushauri wa watalaamu wa kilimo ili kumaliza tatizo la ugonjwa  wa  zao hilo.
Hayo yamebainisha na  Afisa kilimo wa kata ya Katwe katika Halmashauri ya Buchosa wilayani Sengerema mkoani Mwanza Tumaini  William     wakati akizungumza na   Radio Sengerema ofisini  kwake na kusema kuwa  baadhi  ya wakulima wamekuwa  wakilima zao  hilo  bila  kufuata  kanuni na taratibu za  uendeshaji  wa kilimo hali iliyopelekea  kushuka katika uzalishaji  wa zao hilo.

Aidha William ameongeza kuwa  tatizo la ugonjwa wa muhogo   kanda ya ziwa  ni mkubwa kwa mujibu wa tafiti za watalaamu wa chuo cha kilimo cha Ukiliguru  na tiba yake ni    kuzingatia maelekezo ya maafisa ugani .
Na Charles Sungura                   

Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.