RUNGU LA KIPOLE LATUA KWA WAVUVI HARAMU
Image result for picha ya nyavu haramu
nyavu haramu zikiwa zinachomwa
Mkuu wa wilaya ya Sengerema Mkoani Mwanza Mh, Emmanuel Kipole amewataka viongozi pamoja na wananchi wanaojihusisha na uvuvi haramu kuacha mara moja shughuli hiyo ndani ya  ziwa Victoria.
Katika mahojiano na Radio sengerema Mh,Kipole amesema zoezi la kupambana na uvuvi haramu linaendelea na kwamba kiongozi yeyote atakaebainika kushirikiana na wavuvi harama hatua kali zitachukuliwa dhidi yake.
Hata hivyo Mh, Kipole amesema changamoto kubwa  inayowakabili ni wavuvi wa maeneo mengine kuingia katika ziwa la upande wa wilaya ya Sengerema na wanapowaondoa hukimbilia maeneo mengine.
Aidha Mkuu wa wilaya amesema ni wakati muafaka wa wananchi wote wilayani Sengerema kuachana na uvuvi haramu katika ziwa Victoria ili kulinda mazalia ya samaki.
Na Elisha Magege.


Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.