RAIS MAGUFULI AWATAKIA SIKUKUU YA IDD EL HAJJ NJEMA
Image result for picha ya rais

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, amewatakia waumini wa dini ya Kiislam sikukuu njema ya Eid El Hajj.

Katika ukurasa wake wa twitter Rais Magufuli ametoa ujumbe huo wa kuwatakia Eid njema, huku akihimiza kudumisha amani, upendo na mshikamano.


Waumini wa dini ya Kiislam nchini leo wanaungana na Waislam wenzao wote duniani, kusherehekea sikukuu ya Eid El Hajj  ambayo huadhimishwa kila mwaka, mara baada ya ibada ya Hija kukamilika, na mara nyingi husherehekewa kwa kuchinja wanyama waliohalalishwa kwa binadamu.

Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.