ONYO LATOLEWA KWA WAMILIKI WA NYUMBA
Related image
nyumba
Wamiliki wa nyumba za kupangisha Wilaya ya Sengerema wametakiwa kuwatambua mabalozi wa maeneo yao kwa kuwapatia taarifa    mapema  wakati   wanapopata wapangaji na wageni katika nyumba zao.
Tamko hilo limetolewa na mwenyekiti wa kata ya Nyatukara Bwn,Pelana Bagume  wakati alipokuwa kwenye kikao cha ulinzi na usalama ambapo amewatahadharisha wamiliki ambao watabainika kuishi na mpangaji bila  kumtambulisha kwa kiongozi wa mtaa   watachukuliwa hatua kali  pamoja na  mpangaji wake.
Kwa upande wake diwani  wa Kata ya Nyatukara   Mh, salleh msabah  amewatahadharisha wamiliki wa nyumba kuwa kutowatambulisha wapangaji wao kwa viongozi wa maeneo yao ni kosa kisheria hivyo watakaobainika watachukuliwa hatua  za  Kisheria .
Na Said Mahera.


Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.