MATUNDA YAANZA KUONEKANA BAADA YA KUKOMESHA UVUVI HARAMU
Imeelezwa kuwa baada ya serikali kukomesha uvuvi haramu upatikanaji wa samaki Wilayani Sengerema umekuwa mzuri huku wanunuzi wakielezea  jinsi wanavyopata samaki wakubwa tofauti na hapo awali.
Wakiongea na radio sengerema wafanyabiashara wa samaki katika soko la migombani wilayani Sengerema wamesema kwa sasa bei ya samaki mkubwa zaidi ni Tsh 25,000/= huku samaki wa kawaida wakiuzwa sh,6000/= mpaka sh,2000/=
Hata hivyo radio sengerema ikapiga hodi kwa wafanyabiashara wa dagaa ambapo wameelezea jinsi bei  ya biashara hiyo kupanda hadi kufika kisado kuuzwa tsh 9000/= wakati awali kiliuzwa kwa tsh 5000/=huku wakieleza changamoto wanazokumbana nazo  wakati wa uchuuzi wa biashara hiyo kwa wanunuzi.

Kwa upande wao wanunuzi wamesema kuwa wanaipongeza serikali kwa juhudi wanazofanya juu ya wavuvi wanaovua mazalia ya samaki kwa kuwa sasa wanakula samaki wakubwa.

Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.