MATUMIZI MABAYA YA SILAHA YAWAFIKISHA MAKAMANI WATU 3
SILAHA ZA MOTO
Watu  watatu   wamefikishwa   katika   mahakama    ya  wilaya   ya   sengerema   mkoani   mwanza   kwa   tuhuma   ya  makosa   matatu  ya  unyangh’anyi   wa  kutumia  silaha  pamoja   na  kusababisha  maumivu  ya  mwili.
Akisoma  mashitaka   yanayowakabili   mbele    ya  hakimu   wa  mahakama  hiyo  BI   MONIKA  NDYEKOBORA .mwendesha  mashitaka   wa  jeshi  la   polisi  INSPECTA   SLIVESTA  MWAISEJE,amewataja   washitakiwa  kuwa  ni JUMA   KIFONGONYO mwenye   umri   wa   miaka  41  mkazi   wa Lushamba,  MTAKI   LYOMA   maarufu  LUBALAZA mwenye   umri   wa   miaka  45  mkazi   wa   Nyamatongo   na  JASTINE   MTESIGWA mwenye   umri   wa   miaka  40  mkazi   wa  Kamanga.
INSPECTA  MWAISEJE  ,amesema   kuwa  washitakiwa   wote   kwa   pamoja   wanashitakiwa   kwa makosa  matatu  ambapo   kosa  la   kwanza  ni  unyangh’anyi  wa  kutumia  silaha   kinyume   na   kifungu   namba  287  (A) cha  kanuni ya   adhabu   sura  ya   16,kuwa  washitakiwa  wote  kwa  pamoja   wanashitakiwa  mnamo agost  22  mwaka  huu  majira  ya  saa 7:30  usiku  huko  katika   kijiji   cha  nyamatongo   wilayani   sengerema   mkoani   mwanza  waliiba   kiasi   cha   shilingi  milioni  moja  mali   ya  SIMONI  JOHN SANGIJA kabla   na   baada   ya  kufanya   unyangh’anyi   huo   walitumia  silaha   aina   ya  panga  na  nondo   katika   kufanikisha  unyangh’anyi   huo.
Kosa   la   pili   ni  unyangh’anyi   wa  kutumia  silaha ,  kinyume   na   kifungu   namba  287  (A) cha  kanuni ya   adhabu   sura  ya   16,kuwa  washitakiwa  wote  kwa  pamoja   wanashitakiwa  mnamo  tarehe  tajwa  majira   ya   saa 7:40   usiku  huko  katika   kijiji   cha  nyamatongo   wilayani   sengerema   mkoani   mwanza  waliiba   kiasi   cha   shilingi  milioni  moja na  laki  tano  mali   ya MASHILA  MALULA kabla   na   baada   ya  kufanya   unyangh’anyi   huo   walitumia  silaha   aina   ya  panga  na  nondo     katika   kufanikisha  unyangh’anyi   huo.
Kosa  la  tatu  ni  kusababisha  maumivu   ya  mwili  kinyume   na  kifungu  namba  225  cha  kanuni ya   adhabu   sura  ya   16,kuwa  washitakiwa  wote  kwa  pamoja   wanashitakiwa  mnamo  tarehe  tajwa  majira   ya   saa 7:50   usiku  huko  katika   kijiji   cha  nyamatongo  wilayani   sengerema   mkoani   mwanza  walisababisha   maumivu  makali   ya  mwili   kwa  KULWA  WILIAMU MASABA  kwa  kumkata  na  panga  kichwani  na  sehemu  mbalimbali  za  mwili   wake.
Hata  hivyo   washitakiwa  wote  kwa  pamoja   wamekana  kutenda  makosa   hayo  na   watuhumiwa   wamerudishwa   rumande   hadi  septemba  26  mwaka  huu  kesi   hiyo   itatajwa  kwa  maelezo   ya   awali  mahakamani   hapo.


Na Joyce Rollingstone.

Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.