Madawa ya kulevya

MAPAMBANO YA DAWA ZA KULEVYA YANAENDELEA.


Mkuu wa wilaya ya Sengerema mkoani Mwanza  Mh, Emmanuel Kipole amewataka wananchi wote kutoa ushirikiano  ili kutokomeza  biashara  na  matumizi  ya  dawa za kulevya wilayani  Sengerema .
Akizungumza na radio Sengerema Mh, Kipole amesema tangu zoezi la kupinga marufuku matumizi pamoja na biashara  hiyo ya dawa za kulevya nchini  Wilaya ya  Sengerema wamefanikiwa kwa kiwango kikubwa  kudhibiti matumizi ya dawa hizo   na kilimo cha bangi.
Katika hatua nyingine Mh,kipole amesema ni vyema wananchi wote kwa pamoja wakashirikiana kutokomeza biashara ya dawa za kulevya, ili kuondoa vijana tegemezi kataka jamii.
Hivi karibuni    Serikali ya awamu ya tano  imepiga maarufuku     biashara na matumizi ya dawa za kulevya  nchini kwa lengo la kuwaokoa  kundi kubwa la vijana  waliokuwa wametumbukia katika janga hilo.     
Na Elisha Magege.






Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.