MAAMUZI YA KESI YA URAIS NCHINI KENYA LEO KUJULIKANA

Image result for picha ya uhuru kenyatta
Mahakama kuu nchini Kenya leo itatoa uamuzi wa kesi iliyowasilishwa na Muungano wa Upinzani nchini humo wa kupinga Uhuru Kenyatta, kutangazwa tena kuwa mshindi wa Urais.
Muungano huo wa NASA unadai kuwa matokeo ya uchaguzi ya mwezi Agusti yalikuwa na udanganyifu.
Tume ya taifa ya Uchaguzi nchini humo ilimtangaza Uhuru Kenyatta kuwa mshindi wa uchaguzi kwa ushindi wa zaidi ya nusu ya kura zote zilizopigwa na kumshinda mpinzani wake mkubwa, mkongwe wa siasa za upinzani Raila Odinga.
Muungano wa upinzani nchini Kenya unaitaka mahakama kuu kubatilisha matokeo hayo ya uchaguzi wa mwezi uliopita.
Unadai kuwa mitambo ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi IEBC ilidukuliwa na matokeo kuvurugwa.
Upinzani pia unaituhumu Tume ya taifa ya Uchaguzi kwa kutumia namba za kupigia kura ambazo zilikuwa hazijathibitishwa rasmi.
Mahakama inayosikiliza kesi hiyo imeruhusu tayari mawakili wa upinzani kuweza kupata Data na vifaa vilivyotumika katika uchaguzi.

Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.