KAA LA MOTO LAWASHUKIA WASIOWAPATIA MIKATABA WAAJIRIWA WAO
Image result for PICHA EMMANUEL KIPOLE
Ongeza kichwa
                   Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Mh Emmanuel Kipole


Mkuu wa wilaya ya Sengerema Mh Emmanuel Kipole amewataka waajiri wote wilayani Sengerema kuwapatia mikataba watumishi wao wa kazi.

Amesema hayo kufuatia kupokea malalamiko mengi kutoka kwa baadhi ya wananchi ambao hawajapewa stahiki zao na kuwaomba wananchi  kutambua haki zao za msingi pindi wanapoomba ajira ili wapewe msaada wa kisheria pindi inapobainika kuwepo kwa tatizo la kutolipwa stahiki zao ili kuepuka kudhulumiwa.
Mh. Kipole amesema kuwa waajiri na waajiriwa wanatakiwa kujua sheria ya kazi ili kuweza kutekeleza majukumu kati ya mwajiri na mwajiriwa.


Hata hivyo jamii imetakiwa kuzingatia suala la mkataba pale wanapopata ajira ili kuepuka adha inayoweza kutokea.
Na Anna Elias. 

Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.