ELIMU YATAKIWA ZAIDI KWA WAKULIMA NA WAFUGAJI
Related image
mifugo
Wafugaji  na wakulima   wa  kijiji cha Ngoma  Kata ya Igalula wilayani Sengerema mkoani Mwanza wametakiwa kuunda vikundi ili serikali iweze kuwasaidia  kuwa na  ufugaji  wenye  tija.
Hayo  yamebainishwa na Afisa kilimo na mifugo wa Kata ya Igalula  Bwn, Stanley Shija alipoongea na redio Sengerema ofisini kwake  na  kusema wafugaji wakiungana kwa  pamoja watafanikiwa.
Shija amesema maendeleo katika shughuli yoyote  yanapatikana kwa kuwa na malengo na mpango kazi na kuzingatia ushauri wa watalaamu wa kilimo na mifugo.
Katika  hatua nyingine  amewaomba wananchi kutokatishwa tamaa na changamoto za kilimo  ikiwemo  suala  la  hali ya hewa katika msimu wa kilimo  ambazo haziepukiki na zile za pembejeo kwani serikali inajitahidi kuzipatia ufumbuzi.
Image result for picha ya wakulima
mkulima
Aidha  ameongeza kuwa serikali itaweza kuwahudumia wakulima na wafugaji kwa kutoa  elimu na mitaji kwa wananchi walioko kwenye vikundi.      
Na,Charles  Sungura


Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.