CHARLES TIZEBA AWAPONGEZA
WANANCHI KWA KUJITOLEA KUFANYA SHUGHULI ZA KIMAENDELEO

Waziri
wa kilimo,mifugo na uvuvi ambae pia ni Mbunge wa Jimbo la Buchosa wilayani
Sengerema Mh, Charles Tizeba amewapongeza
viongozi na wananchi wa kata za Bupandwamhela
na Kafunzo kwa jitihada walizo
onesha katika uboreshaji wa miundo mbinu pamoja na vituo vya afya katika kata
zao.
Pongezi
hizo amezitoa katika mkutano wake wa hadhara wa kuwashukuru wananchi wa kata
hizo kwa kuendelea kumuamini na kumpa kura katika uchaguzi mkuu uliofanyika
mwaka 2015.
Kwa
upande wake Makamu mwenyekiti wa Halmashauri ya Buchosa Mh, Idama Kibanzi amewapongeza
viongozi wa vijiji vilivyotekeleza ujenzi wa zahanati kwani mpaka sasa vijiji
vingi katika Jimbo la Buchosa vimeanza kutekeleza ilani ya chama cha mapinduzi.
Hata
hivyo Madiwani wa kata hizo mbili Mh,Dotto Fransis Bulunda wa kata ya
kafunzo na Mh,Masumbuko Bupamba wa
kata ya Bupandwa wamemushukuru mbunge wa jimbo hilo kwa jitihada anazo onyesha
za kuwaunga mkono wananchi wa jimbo lake.
Aidha
Mh, Tizeba amewataka viongozi wote
wa vijiji kuhakikisha wanawahamasisha wananchi kushiriki katika shughuli za
maendeleo na katika kata zote hizo mbili ameahidi mifuko ya saruji, matofari na
mabati kwa lengo la kuwaungo mkono wananchi na viongozi wa kata hizo ili
kuchochea maendeleo katika kata hizo.
Na Elisha Magege.
Comments
Post a Comment