ASIMAMISHWA KAZI KISA MIGOGORO YA ARDHI
Kiwanja

Mkuu wa mkoa wa Mwanza John Mongela leo amesikiliza kero mbalimbali za ardhi kwa  wakazi wa wilaya ya Ilemela Jijini Mwanza huku akimsimamisha kazi ili  kupisha uchunguzi mthamini wa ardhi wa halmashauri ya Jiji la Mwanza.

Mthamini huyo aliyefahamika kwa majina ya Egbert Rwabukabwa ambaye ni mthamini daraja la pili wa halmashauri ya Jiji la Mwanza amesimamishwa kazi baada ya mkazi mmoja wa wilaya hiyo kudai kuwa kuna eneo lake ambalo amemilikishwa mtu mwingine.

Kutokana na hilo mkuu wa mkoa wa Mwanza amemuagiza katibu tawala kumsimamisha kazi mthamini huyo ili kupisha uchunguzi na kutoa rai kwa watumishi wa idara ya ardhi kufanya kazi kwa uaminifu

Leo september  13 mkuu wa mkoa wa Mwanza John Mongela amesikiliza kero mbalimbali za wananchi wa wilaya ya Ilemela kutokana na kuwepo kwa malalamiko mengi ya wananchi kuhusu ardhi.


 Na Veronica Martine

Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.