AFARIKI DUNIA AKIOGELEA NDANI YA ZIWA VICTORIA
picha ya ziwa victoria
Mtu mmoja amefariki na wengine watatu kunusurika wakati wakiogelea katika ziwa Victoria katika  kijiji  cha Luchili kata ya Nyanzenda Halmashauri ya Buchosa wilayani Sengerema.
Aliye patwa na mauti hayo amejulikana kwa ya Thobias martine mwenye umri wa miaka 33 mkazi wa kitongoji cha kabapani kilichopo katika kijiji na kata ya Nyanzenda.
Chanzo cha tukio imeelezwa kuwa Thobias pamoja na wenzake watatu walikuwa wakivua samaki katika ziwa Victoria kwa kutumia ndoano  na ilipo fika jioni waliamua kutoka ziwani kwa kuogelea kutoka kwenye jiwe ambalo walikuwa wakilituimia kuvulia samaki na kuelekea nchi kavu ndipo Thobias alipo zidiwa na maji na khari hiyo ikamsababishia kuzama.
Baraka Pascal mwenye umri wa miaka 16,David Hamli miaka 17 na mwingine  aliye fahamika kwa jina moja la Charles mwenye umri wa miaka 13 ni wahanga wa tukio hilo na  hapa wanasimlia njisi tukio hilo ambavyo limetokea.
Happyness Deus ni mke wa marehemu na hapa anaelezea njisi mumewe alivyo ondoka nyumbani na kuelekea katika shughuri zake za kila siku.
Kwa upande wake mwenyekiti wa kijiji hicho Ibrahimu Mbata amedhibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuwataka maafisa Uvuvi kutoa elimu kwa wavuvi  ili wavuvi watambue mambo mhimu wanayo paswa kuzingatia kabla hajaingia katika shughri zao za uvuvi
Na Katemi Lenatus.                        


Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.